SABABU KWA NINI UTUMIE MITANDAO YA KIJAMII KUTANGAZA BIASHARA NA SHUGHULI ZAKO:
Kabla ya kukua kwa matumizi ya Intaneti, Biashara na Shughuli nyingi zilitumia mbinu ya moja kwa moja( offline marketing tactics) kujitangaza. Kadri matumizi ya Mtandao wa Intaneti yalivyoongezeka kila mtu mwenye biashara na shughuli inayotakiwa kujulikana kwa watu alianza na kuendelea kutumia ili kuwafikia Wateja kwa Urahisi na kwa haraka sana. Tumeona Makampuni Makubwa kwa Madogo na Taasisi mbalimbali zikifungua wovuti binafsi kuwakirisha shughuli zao. Wovuti hizi zilianzishwa kiutaalamu zikisimama juu kwenye Injini za Utafutaji ( Search Engines) na Maneno Muafaka ( specific keywords).